.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumapili, 25 Mei 2014

HARUSI YA KANYE WEST NA KIM KARDASHIAN YAFUNGWA JUU YA KILIMA NA KUHUDHURIWA NA WAGENI 600

Kanye West na Kim Kardashian wamefunga ndoa kwa kufanya harusi ya kifahari nchini Italia hapo jana, huku Kanye akimtambulisha kwa wageni Kim kama 'my baby, Kim Kardashian West'.

Mabilionea kadhaa waliohudhuria harusi hiyo walishuhudia wanandoa hao wakila kiapo kwenye kilele cha kilima katika mji wa Florence huku wakikingwa na ukuta wa kutengeneza wenye urefu wa futi 20 uliopambwa mau, wakati jua likianza kuzama.

Wanandoa hao wapya walionekana wakiwa wamekumbatiana kwa furaha wakiangalia wageni wao wapatao 600, waliowaalika bila ya kuwepo rafiki wa Kanye Beyonce na Jay Z pamoja na kaka wa Kim aitwae Rob.
              Eneo la Kilimani lililofanyika harusi ya Kanye na Kim wakati likijengwa
           Kaka wa Kim Kardashian aitwae Rob hakuhudhuria harusi ya dada yake
                                                   Wageni waalikwa wakielekea kwenye harusi
                          Wageni waalikwa wakielekea kwenye harusi 
         Kanye, Kim, Baby North na Mama Mkwe Kris Jenner 

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni