.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumapili, 25 Mei 2014

MAHAKAMA YATENGUA UAMUZI WA RAIS BANDA KUFUTA MATOKEO YA UCHAGUZI MKUU

Mahakama Kuu ya Malawi imekataa uamuzi wa Rais Joyce Banda kufuta uchaguzi wa mkuu uliofanyika wiki hii, ambapo yeye pia alikuwa mgombea.

Awali Bi. Banda alisema uchaguzi uliofanyika siku ya jumanne uligubikwa na udanganyifu, vitendo vya upigaji kura mara mbili pamoja na kufanyiwa uharamia wa kwenye komputa.

Rais Banda alisema kuwa uchaguzi huo utarudiwa ndani ya siku 90 na hatogombea tena katika uchaguzi mpya.

Hata hivyo Mkuu wa Tume ya Uchaguzi ya Malawi amesema rais Banda hana madaraka ya kuufutilia mbali uchaguzi huo, na Mahakama Kuu imetengua uamuzi wa Rais Banda na kura zitaendelea kuhesabiwa.

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni