.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumanne, 27 Mei 2014

MWANAMKE MUINGEREZA AJULIKANAE KAMA MJANE MWEUPE AOLEWA NA KIONGOZI WA AL SHABAAB

Mwanamke raia wa Uingereza Samantha Lewthwaite aliyepachikwa jina la Mjane Mweupe ameolewa na kiongozi mkatili wa kundi la al Shabaab la Somalia.

Vyanzo vya habari vimesema mkimbizi huyo Muingereza amemuoa mtuhumiwa huyo mbabe wa vita Hassan Maalim Ibrahim ambaye pia hujulikana kama Sheikh Hassan, hii ikiwa ni ndoa yake ya tatu.

Sheikh Hassan ni kiongozi mwandamizi wa kundi la kikaidi la al-Shabaab ambalo linauhusiano na al-Qaeda, na sasa Samantha Lewthwaite atakuwa akipewa ulinzi mkali kutokana na kuwa ni mke wa kiongozi.

Kwa mara ya mwisho Samantha Lewthwaite alionekana katika utekaji wa duka kubwa la bidhaa Jijini Nairobi akiwaongoza watekaji nyara ambao waliua watu 67 na inaaminika waliishia kujilipua na kujitoa mhanga.
Samantha Lewthwaite ni mjane wa mlipuaji wa tukio la 7/7 Germaine Lindsay ambaye aliuwa watu 26 kwenye treni ya aridhini huko London, Julai 2005.
                                                         al- Shabaab wakiwa mazoezini



Hakuna maoni :

Chapisha Maoni