.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumanne, 27 Mei 2014

MWANAMUZIKI WA KUNDI LA GOODLYFE ALIVYOKAMATWA NA POLISI WA UGANDA KWA UGOMVI KATIKA BAA



Mwanamuziki nyota wa Uganda wa kundi la Goodlyfe Mowzey Radio jana asubuhi alijikuta akizolewa mzobe mzobe na polisi nyumbani kwake kufuatia ugomvi uliotokea kwenye baa ya Casablanca.

Ugomvi huo ulisababishwa na kundi la Team No Sleep ambalo linaundwa na wasanii waliojitenga lebo ya Leone Island ambao ni AK47 pamoja na kaka yake mkubwa Pallaso Sheebah Kalungi na King Saha.

Kisa cha ugomvi huo ni kauli ya mmoja wa watu wa kundi la Radio kudai kuwa kama si kwa kundi la Goodlyfe ngoma ya AK47 na Pallaso ya Amaaso isingetamba jambo ambalo lilimkera na kumuita kaka yake Pallaso ambaye alienda moja kwa moja kwenye meza ya kina Radio na kuipiga ngumi.
Ndani ya gari la polisi  
                       Polisi waking'oa bangi katika nyumba ya Mowzey Radio
                           Mowzey Radio akiwa na Chagga, Meneja Mpya wa Kundi la Goodlyfe

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni