.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumatatu, 26 Mei 2014

PAPA FRANCIS KUTEMBELEA ENEO LA KUMBUKUMBU YA MAUAJI YA WAYAHUDI

Papa Francis atatembelea eneo la kumbukumbu ya kitaifa ya mauaji ya kikatili ya halaiki ya Wayahudi huko Yad Vashen, katika siku yake ya mwisho ya ziara ya siku tatu Mashariki ya Kati hii leo.

Baada ya kuwasili Israel jana, Papa alielezea mauaji hayo ya kuchomwa moto Wayahudi yanayojulikana kwa jina la Holocaust, kama alama isiyovumilika inayoonyesha ni kwa kiasi gani binadamu anaweza kufanya kitendo cha kishetani.

Hii leo pia Papa Francis anatarajiwa kutembelea maeneo ya kidini huko Jerusalem na kufanya maongezi viongozi wakuu wa dini nchini Israel.

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni