.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumatatu, 26 Mei 2014

SENETA WA JIJI LA NAIROBI ADAI MAISHA YAKE YAPO HATARINI BAADA YA KUIBUKA UGOMVI NA MBUNGE MWANAMKE





                            Seneta Sonko akiwa katika pozi na mbunge Rachael Shebesh 
Seneta wa Jiji la Nairobi Mike Mbuvi Sonko amedai kuwa maisha yake yapo hatarini kufuati madai ya kuwepo kwa ugomvi baina yake na Mbunge Mwakilishi wa Wanawake Rachael Shebesh katika baa moja siku ya jumamosi.

Seneta huyo ametoa madai hayo kwenye ukurasa wake wa Facebook, saa kaadhaa kupita tangu kutokea kwa ugomvi huo ambao uliambatana na kufyatuliwa kwa risasi. Sonko aliandika taarifa yake katika kituo polisi cha Kilimani usiku huo huo wa tukio.

Wanasiasa hao wawili wameagizwa kuripoti Ofisi ya Mpelelezi wa Makosa ya Jinai katika kituo cha Kilimani hii leo.

Wakati hayo yakijiri picha zinazomuonyesha Seneta Soko na Mbunge Shebesh wakiwa wamekaa katika pozi linaloashiria kuwa na uhusiano wa karibu mno zimekuwa zikisambwazwa kwenye vyombo vya habari.


Hakuna maoni :

Chapisha Maoni