Katika mchezo huo ilibidi Ghana wapambane kufa na kupona ili kuhakikisha wanasonga mbele baada ya kuwa wametangulia kufungwa bao katika dakika ya 17 ya kipindi cha kwanza na mchezaji mahiri wa Afrika Kusini, Masango.
Bao hilo lilidumu hadi kipindi cha kwanza kinamalizika. Kipindi cha pili ndipo Ghana walipofanikiwa kupata mabao hayo mawili katika dakika za 73 na 83 wafungaji wakiwa ni Boye na Andre Ayew.
Kwa matokeo hayo Ghana imesonga mbele hatua ya robo fainali baada ya kumaliza ikiwa inaongoza kundi C kwa kuwa na pointi 6.

Hakuna maoni :
Chapisha Maoni