Fainali za mataifa Afrika 2015 ( AFCON ) zinazoendelea kutimua vumbi nchini Equatorial Guinea zinaendelea leo kwa mechi za kundi A.
Katika kundi hilo lenye nchi za Gabon, Equatoria Guinea, Congo na Burkina Faso, mchezo wa kwanza utakuwa kati ya wenyeji Equatorial Guinea ambao watacheza na Burkina Faso na kufuatiwa na mechi kati ya Gabon na Congo.
Katika kundi hili mpaka sasa Gabon inaoongoza ikiwa na pointi 3 ikifuatiwa na Equatoria Guinea yenye pointi 1 sawa na Congo yenye pointi 1 na Burkina Faso ikiwa haina pointi.

Hakuna maoni :
Chapisha Maoni