Serikali ya China imewasilisha rasmi
ombi la kuitaka nchi ya Kenya, kuwakabidhi kwao wachina 76 ambao
wanakabiliwa na kesi ya uhalifu wa kimtandao Jijini Nairobi.
Watuhumiwa hao walikamatwa Jijini
Nairobi, wameiba shilingi bilioni 1.5 za Kenya kwa watu mbalimbali
nchini China kwa kutumia njia ya mtandao, mamlaka za China zimesema.
Balozi wa China nchini Kenya, Liu
Xianfa, ameiandikia barua Wizara ya Mambo ya Nje akitaka watuhumiwa
hao wakabidhiwe China kutokana na uchunguzi kubaini wote walioibiwa
fedha hizo ni raia wa China.

Hakuna maoni :
Chapisha Maoni