.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumapili, 25 Januari 2015

FAINALI ZA MATAIFA AFRIKA 2015, IVORY COAST YAPONEA CHUPU CHUPU KWA MALI

Fainali za mataifa Afrika zimeendelea kutimua vumbi nchini Equatorial Guinea hapo jana kwa kushuhudia mechi za kundi D ambazo zote zilimalizika kwa kugawana pointi. 

Katika mchezo uliozikutanisha Ivory Coast na Mali, nchi hizo zilitoka uwanjani zikiwa zimefungana bao 1-1.
Mali ndio waliokuwa wa kwanza kupata bao lililofungwa kunako dakika ya 6 na mchezaji Bakary Sako, bao ambalo lilidumu hadi kipindi cha kwanza kinamalizika. 

Kipindi cha pili kilianza kwa kasi na ilionekana wazi jahazi la Ivory Coast lilikuwa linataka kuzama kutokana na kuelemewa na Mali. 

Lakini katika dakika ya 86 ya mchezo, Max Gradel aliisawazishia Ivory Coast na kufanya matokeo kuwa 1-1.

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni