Cameroon na Guinea zimetoka uwanjani zikiwa zimefungana bao 1-1 katika mchezo wa kundi D wa kuwania kombe la Mataifa ya Afrika, katika fainali zinazoendelea nchini Equatorial Guinea.
Katika mchezo huo Cameroon ndio waliokuwa wa kwanza kutikisa nyavu za wapinzani wao katika dakika ya 13 mfungaji akiwa ni Benjamin Moukandjo.
Hata hivyo dakika chache kabla ya mpira kuwa mapumziko, mshambuliaji wa Mali, Ibrahima Traore allisawazishia timu yake.
Hadi mwisho wa mchezo timu hizo zilitoka uwanjani zikiwa zimefungana bao 1-1.
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni