.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumapili, 25 Januari 2015

CRISTIANO RONALDO ALAMBWA KADI NYEKUNDU KWA KUGEUZA SOKA KUWA NGUMI

Mchezaji nyota wa Real Madrid Cristiano Ronaldo amejikuta matatani baada ya kugeuza mchezo wa soka kuwa wa ngumi na mateke hapo jana kwa kumpiga mchezaji Edimar katika mchezo wa La Liga.

Hii ni mara ya kumi kwa mwanasoko huyo bora wa mwaka wa dunia kutolewa nje kwa kadi nyekundu katika maisha yake ya soko la kimataifa.

Ronaldo aliyeonekana kukereka alitenda kosa hilo dakika ya 83, wakati Real na Cordoba zikiwa sare ya bao 1-1, hata hivyo Gareth Bale alifunga bao katika dakika za mwisho na kuipatia Real ushindi.

Baada ya tukio hilo, Ronaldo alitwitti katika twitta yake maneno yasemayo anaomba msamaha kwa kila mtu na hususan kwa Edimar kwa kitendo kisichofikirika alichokifanya katika mchezo huo.
                 Cristano Ronaldo alipogeuka Bruce Lee kwa kumpiga ngumi pia Jose Angel Crespo
                       Edimar akianguka chini baada ya kupigwa teke na Cristiano Ronaldo
                                            Cristiano Ronaldo akilambwa kadi nyekundu na refa

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni