.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumanne, 20 Januari 2015

FAINALI ZA MATAIFA AFRIKA 2015, SENEGAL YAIFUNDISHA SOKA GHANA

Mchezaji wa Ghana, Andrew Ayew akikimbia kwa furaha baada ya kuifungia timu yake bao la kuongoza kwa mkwaju wa penati dhidi ya Seneagal. 

Timu ya taifa ya Ghana jana ilikumbana na kipigo cha mabao 2-1 toka kwa Senegal katika mchezo wa kundi C wa michuano ya fainali za Mataifa ya Afrika zinazoendelea nchini Equatorial Guinea.
Pamoja na kutangulia kupata bao kwa njia ya penati katika dakika ya 14 ya mchezo kupitia kwa Andrew Ayew, Ghana walishindwa kulilinda bao hilo na kujikuta wakimaliza mchezo huku wakiwa wamefungwa mabao 2-1.
Mabao ya Senegal, maarufu kwa jina la Simba wa Teranga inayoonekana kuimarika sana katika fainali hizi yaliwekwa kimiani na wachezaji Biram Diofu katika dakika ya 58 na bao la pili nala ushindi likifungwa na Moussa Sow dakika ya 90 ya mchezo huo.
Kwa matokeo hayo, Algeria inaongoza kundi C ikiwa na pointi 3 sawa na Senegal lakini ikiwa na mabao zaidi, huku Ghana wakiwa nafasi ya tatu na Afrika Kusini wakiwa mkiani

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni