Wakili wa hoteli
inayodaiwa kupora ardhi ya eneo la michezo la watoto wa shule ya
msingi ya barabara ya Lang'ata Jijini Nairobi amesema kuwa Naibu Rais
wa Kenya William Ruto si mmiliki wa hoteli hiyo.
Sakata la kuvamiwa
kwa eneo hilo jana lilipelekea kujeruhiwa kwa wanafunzi watano na
polisi mmoja baada ya polisi kufyatua mabomu ya machozi kwa watoto,
walimu wao na wanaharakati walioandamana kupinga uvamizi huo.
Kufuatia tukio
hilo wananchi Kenya walimelikosoa jeshi la polisi kwa kutumia nguvu
kubwa dhidi ya watoto, jambo ambalo limeilazimu polisi kutoa taarifa
ya kumsimamisha kazi afisa aliyesimamia operesheni hiyo OCPD Elija
Mwangi.


Hakuna maoni :
Chapisha Maoni