.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumanne, 13 Januari 2015

KAMANDA MWANDAMIZI WA LRA ONGWEN AWATAKA WENZAKE WAJISALIMISHE

Mmoja wa Makamanda waandamizi wa kundi la waasi la Lord's Resistance Army (LRA) la nchini Uganda, Dominic Ongwen, ambaye amejisalimisha kwa majeshi ya Marekani amewataka makamanda za zamani wa kundi hilo kujisalimisha na kutoka msituni na kumaliza uasi.

Ongwen ambaye anakabiliwa na mashitaka katika mahakama ya kimataifa ya makosa ya uhalifu ICC alikamatwa wiki iliyopita nchini Afrika ya Kati (CAR) na kusema kwamba pia amepokea msamaha kutoka kwa rais wa Uganda Yoweri Museveni ingawa serikali ya Uganda haijasema lolote kuhusu kauli hiyo.

Kundi la LRA limekuwa likilaumiwa kwa kuuwa watu zaidi ya 100,000 na kuteka watu zaidi ya 60,000 ikiwa ni pamoja na watoto katika mapambano yaliyodumu kipindi cha miongo mitatu katika nchi tano za Afrika ya Kati.

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni