Katika mchezo huo wa ligi kuu nchini Uingereza, Chelsea walionekana tangu mwanzo wa mchezo kuwa wamepania kuibuka na ushindi mnono.
Kwa matokeo hayo, Chelsea wameendelea kujikita kileleni baada ya kufikisha pointi 52 wakizidi kuwakimbia mabingwa watetezi, Manchester City walio nafasi ya pili wakiwa na pointi 47.
Mabao ya Man United yaliwekwa kambani na wachezaji
Marouane Fellaini katika dakika ya 58 na bao la pili likifungwa na James Wilson katika dakika ya 90.
Pamoja na ushindi huo, Manchester United wamesimama nafasi ya nne wakiwa na pointi 40 huku Southamton wakiwa nafasi ya tatu wakiwa na pointi 42.
Liverpool nayo jana ilifanikiwa kupata pointi tatu muhimu na kufikisha jumla ya pointi 35 wakiwa nafasi ya saba katika msimamo wa ligi kuu Uingereza baada ya kuifunga Aston Villa mabao 2-0.
Liverpool nayo jana ilifanikiwa kupata pointi tatu muhimu na kufikisha jumla ya pointi 35 wakiwa nafasi ya saba katika msimamo wa ligi kuu Uingereza baada ya kuifunga Aston Villa mabao 2-0.
Aston Villa wakicheza katika uwanja wao wa nyumbani, walishindwa kuwazuia Liverpool kuwafunga katika mchezo huo.
Mabao ya Liverpool yalifungwa na Fabio Borini katika dakika ya 24 na bao la pili likifungwa na Rickie Lambert katika dakika ya 79.
Matokeo ya michezo mingine ya ligi kuu Uingereza iliyochezwa jana ni kama ifuatavyo:-
Newcastle 1 vs 2 Southampton
Tottenham 2 vs 1 Sunderland
Leicester 0 vs 1 Stoke
Burnley 2 vs 3 Crystal Palace



Hakuna maoni :
Chapisha Maoni