.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumamosi, 17 Januari 2015

LIGI KUU UINGEREZA KUENDELEA LEO KATIKA VIWANJA SABA TOFAUTI

Ligi kuu nchini Uingereza itaendelea leo katika viwanja saba tofauti. Wakati mabingwa watetezi wa kombe hilo Manchester City wao wakisubiri kushuka dimbani kesho jumapili kuwaalika Arsenal katika uwanja wa Etihad  mchezo ambao unasubiriwa kwa hamu kubwa na mashabiki wa soka kote ulimwenguni, leo vinara wa ligi hiyo Chelsea watakuwa ugenini kucheza na Swansea. 

Mchezo huu unatarajiwa kuwa mgumu kutokana ugumu wa kufungika kirahisi kwa Swansea. 

Michezo mingine ya ligi kuu hii leo, Aston Villa watakuwa nyumbani kucheza na Liverpool, wakati wenyewe Manchester United watasafiri kuwafuata QPR. 

Burnley watakuwa nyumbani kucheza na Crystal Palace na Leicester watateremka dimbani kucheza na Stoke. 

Mchezo mwingine leo ni kati ya Tottenham dhidi ya Sunderland na Newcastle watacheza na Sunderland.

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni