
MAGARI madogo ya abiria katika jiji la Arusha maarufu kwa jina la vifodi, leo yamegoma kutoa huduma wakipinga kutumia utaratibu mpya wa njia ndefu na kuzua vurugu kubwa kati kati ya jiji, huku wananchi wengi wakitembea kwa miguu umbari mrefu.
Vurugu hizo, zimekuwa zikisababishwa
na makundi ya vijana wapiga debe, kuvunja vioo vya magari ambayo
yalikuwa yamekaidi msimamo wa mgomo na kusababisha askari wa FFU
kuingilia kati kuwatawanya.
Mamia ya abiria, wakiwepo wanafunzi
na wafanyabiashara, leo wamelazimika kutembelea kwa miguu na wengine
kukodi pikipiki maarufu kama boda boda.
Katika barabara za Sokoine,Arusha-
Babati ambapo magari ya Njiro- Stendi ndogo, Kwa mrombo- Samunge na
Majengo- Kituo na Fire-Stendi ndogo Kijenge- mjini na maeneo
mengine magari ambayo hufanya safari yalikuwa hayapo barabarani.
Mmoja wa madereva wa daladala, John
Mathias amesema wanapinga kutumia njia ndefu, kwani stendi mpya ya
Samunge haina vyoo na pia hakuna maeneo ya vituo vipya vilivyotengwa
katika njia hizo na hata ikinyesha hakuna mahali pa kujificha
kujikinga na mvua.
Kutokana na mgogoro huo, maafisa wa
jiji la Arusha, chama cha wasafirishaji na Mamlaka ya udhibiti wa
usafiri wa nchi kavu na majani (SUMATRA) wamekutana kwa dharura na
baada ya kikao, waliazimia utaratibu mpya kuendelea.
Jiji la Arusha litaanza rasmi
kutekeleza maazimio ya wadau wa usafiri wa daladali kwa kuanzisha
njia ndefu wenye lengo la kuondoa msongamano wa daladala katikati ya
Jiji jana.
Mwenyekiti wa Kamati ya Mipango Miji
na ni Diwani wa Kata ya Moshono, Paul Matthysen amesema utaratibu wa
njia ndefu ndio suluhu ya msongamano wa magari kati kati ya jiji.
Makubaliano hayo, yameridhiwa na
wasafirishaji, Mamlaka ya Usimamizi na Udhibiti wa Usafiri wa Nchi
Kavu na Majini(Sumatra) ,Baraza la Huduma za Wasafiri (Sumatra CCC),
Halmashauri ya Jiji la Arusha na polisi wa usalama barabarani.
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni