Katibu Mkuu wa Chama cha Mapinduzi
(CCM), Abdulrahamani Kinana, amesema mara baada ya kusaini mkataba wa
kuacha mapigano Sudani Kusini, Tanzania inatarajia kuwapeleka
waadishi wa habari wa vyombo mbalimbali nchini Sudan Kusini, ili
kujifunza athari za vita
vilivyotokea kwa ajili ya kugombea
madaraka.
Akizungumza leo Jijini Arusha,
kabla ya kusaini makubaliano hayo, aliwaambia waandishi wa habari
kuwa wajiandae kwenda Sudani Kusini ili wakajifunze athari za vita
kwa ajili ya kuelimisha wananchi na viongozi.
Amesema katika kuonyesha kuwa
amedhamiria kuwahakikisha waandishi wanapata uelewa wa kutosha katika
kuandika na kutangaza madhara ya vita vya wenyewe kwa wenyewe, Kinana
ameahidi kuwa atahakikisha anawapeleka waandishi wa habari wa Arusha
waitembelee Sudan Kusini.
Amesema anaamini watakapokwenda
kujionea kwa macho madhara ya vita wataweza kutumia vema kalamu zao
kuelimisha watanzania madhara ya vita.
Kinana alisema kwa kuwa wao kupitia
chama cha Mapinduzi (CCM) kiliombwa kufanya mazungumzo juu ya vita
hiyo na ndivyo watakavyofanya pia kwa waandishi ili wapate
somo,”alisema.
Amesema mapigano hayo uyamesababisha
uchumi wan chi hiyo kurudi nyuma, ukizingatia kuwa wao ni wazalishaji
wakubwa wa ng’ombea na watatu katika nchi za Afrika kwa kuwa na
idadi kubwa ya mifugo.
Kinana amesema lakini kwa sababu ya
vita idadi ya mifugo hiyo imepungua kwa kiasi kikubwa huku uchumi wan
chi ukiyumba na kusababisha umaskini kwa wananachi.
amesema Sudan Kusini ilihangaika
miaka zaidi ya 50 kutafuta uhuru wao, miaka miwili baada ya kujitenga
kutoka Sudan Kaskazini, baada ya asilimia 90% kupiga kura ya
kujitenga wakaanza vita ya kugombea madaraka, sasa kila familia
imeathirika kutokana vita ndio wanasaka amani.
Mazungumzo ya kutafuta amani kwa
nchi hiyo yalianza mapema Desemba 23 na 24 mwaka jana 2014 katika
hotel ya Ngurudoto, Wilayani Arumeru, Mkoan Arusha, huku
zikiwakutanisha pande zote tatu zinazopigana kwa ajili ya kusaka
madaraka.
Katika mazungumzo hayo mwenyekiti wa
mazungumzo hayo ni Balozi Dk. Samweli Malecela, ambaye pia alikuwa
ni Waziri Mkuu Mstaafu awamu ya pili ya uongozi wa Rais Ally Hassan
Mwinyi.
Mapigano hayo ya ndani ya chama cha
SPLM katika nchi ya Sudani Kusini yanayohusish makundi matatu ambapo
kila kundi linataka madaraka ya kuongoza nchi hiyo.

Hakuna maoni :
Chapisha Maoni