.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Ijumaa, 30 Januari 2015

MTU MWENYE BASTOLA FEKI ASITISHA MATANGAZO YA TV NCHINI UHOLANZI

Mwanaume mmoja aliyekuwa na bastola feki, amekamatwa baada ya kuvamia studio za kituo cha televisheni ya taifa ya Uholanzi ya NOS, na kupelekea taarifa ya habari ya usiku kutorushwa.

Mwanaume huyo aliyevalia vizuri akiwa ameshika mkononi bastola hiyo refu yenye kiwambo cha kuzuia sauti, alifanikiwa kupenya na kuingia studio, na kushinikiza apewe muda wa kuongea hewani.

Kufuatia tukio hilo kituo hicho cha TV cha NOS, kililazimika kuzima matangazo yake kwa muda wa saa moja, lakini kamera ziliendelea kumrekodi mwanaume huyo hadi pale polisi walipofika na kumkamata.
                     Mtu huyo akiwa amenyanyua mikono baada ya polisi kuingia studio
                                                           Polisi wenye silaha wakimsogelea mtu huyo 
              Polisi wakimkandamiza chini ya sakafu mtu huyo ili kumfunga pingu

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni