Watu wapatao 26 wamekufa katika
mashambulio ya mfululizo yaliyofanywa na wapiganaji kaskazini mwa
Penusula ya Sinai nchini Misri.
Bomu lililotegwa kwenye gari pamoja
na kombora lililolenga wanajeshi, kaskazini mwa Sinai mji mkuu wa
El-Arish limeuwa idadi kadhaa ya wanajeshi.
Mashambulio mengine yametokea karibu
na mji wa Sheik Zuwayid na katika mji wa Rafah, unaopakana na Gaza.
Kundi la wapiganaji la Ansar Beit
al-Maqdis, ambalo linaushirikiano na kundi la Dola ya Kiislam (IS)
limesema limetekeleza mashambulio hayo.

Hakuna maoni :
Chapisha Maoni