Aliyekuwa mwanasayansi katika
maabara ya taifa ya Los Alamos ya Marekani amehukumiwa kifungo cha
miaka mitano jela kwa kujaribu kutoa siri za kutengeneza bomu la
nyuklia kwa nchi za Venezuela.
Mwanasayansi huyo Pedro Leonardo
Mascheroni, alikiri kosa hilo mnamo mwaka 2013, la kutoa siri kwa
jasusi wa shirika la ujasusi la Marekani la FBI, ambaye alijifanya
kuwa ni afisa kutoka Venezuela.
Pedro Mascheroni, mwenye umri wa
miaka 79, anayetokea nchini Argentina, pia mkewe alihukumiwa kifungo
cha mwaka mmoja jela.

Hakuna maoni :
Chapisha Maoni