.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Alhamisi, 15 Januari 2015

PAPA FRANCIS AELEKEA NCHINI UFILIPINO KUANZA ZIARA YA SIKU TANO

Papa Francis anaelekea nchini Ufilipino kwa ajili ya ziara ya siku tano ambayo inangojewa kwa hamu na taifa hilo lenye waumini milioni 80 wa Kanisa Katoliki.

Katika ziara hiyo jambo kuu linalongojea ni mkusanyiko mkubwa wa watu katika misa ya wazi, itakayofanyika katika Jiji la Manila siku ya jumapili.

Pia Papa Francis ataenda eneo la Tacloban kukutana watu walionusurika na kimbunga kilicholeta maafa mwezi Novemba mwaka juzi.

Ulinzi mkali umeimarishwa baada ya majaribio mawili yaliyoshindwa ya kutaka kuwauwa mapapa waliopita.

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni