Shirika la Afya Dunia (WHO)
limeandaa mpango wa kujifanyia mabadiliko, kwa kukiri kuwa
lilichelewa mno kukabiliana na mlipuko wa ugonjwa hatari wa Ebola
Afrika Magharibi.
Katika mkutano wa dharura Jijini
Geneva, Mkurugenzi Mkuu wa WHO, Margaret Chan amesema mlipuko huo wa
Ebola, umeifundisha dunia namna inapaswa kuwajibika katika siku za
baadae.
Zaidi ya watu 8,500 wamekufa kwa
mlipuko wa ugonjwa wa Ebola, wengi wao wakiwa ni wa nchini Sierra
Leone, Guinea pamoja na Liberia.


Hakuna maoni :
Chapisha Maoni