.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Alhamisi, 15 Januari 2015

WACHEZAJI WAKOSA VYUMBA VYA KULALA NCHINI EQUATORIAL GUINEA

Timu zinazowasili kwa ajili ya michuano ya Kombe la Mataifa ya Afrika nchini Equatorial Guinea zimekuwa zinatafuta malazi kutokana na kutokuwepo kwa vyumba vya kutosha vya hoteli.

Kocha wa timu ya taifa ya Congo, Claude Le Roy amesema wachezaji wake watano kati ya 35 hawajapata vyumba vya kulala.

Le Roy amebainisha kuwa wachezaji wengine wa timu yake wanalala kwenye hoteli zisizo na maji, na zenye nywaya za umeme zilizowazi.


Kocha wa Burkina Faso, Paul Put pia amekosoa miundombinu ya malazi ya nchi hiyo mwenyeji wa michuano ya kombe la Mataifa ya Afrika na kusema michuano hiyo ingepaswa kuhairishwa hadi mwezi Juni.

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni