Wachunguzi wa Indonesia wamesema
kuanguka kwa ndege ya AirAsia QZ85501 hakuhusiani na ugaidi, ikiwa ni
kauli ya kwanza kutolewa baada ya kutathimini kisanduku cha taarifa
za ndege.
Mchunguzi wa usalama wa usafiri
Andreas Hananto ameviambia vyombo vya habari kuwa kunadalili kuwa
ndege hiyo ilikumbana na hali mbaya ya hewa na kuanguka.
Ndege hiyo inadhaniwa kuwa ilianguka
Desemba 28 wakati ilipokutana na hali mbaya ya hewa wakati ikikatiza
katika mvua kubwa.
Abiria wote 162 waliokuwemo kwenye
ndege hiyo iliyokuwa ikitokea Surabaya Indonesia kwenda Singapore
walifariki dunia.


Hakuna maoni :
Chapisha Maoni