.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumatano, 28 Januari 2015

WANAWAKE WANAOTUMIA VIDONGE VYA DEPO PROVERA WAPO HATARINI KUUGUA UKIMWI

Ushahidi mpya unaonyesha wanawake wanaotumia vidonge vya mpango wa uzazi aina ya Depo Provera, wapo katika hatari kubwa ya kupata maambukizi ya Ukimwi, na kuzidi kuungana na matokeo ya utafiti uliofanyika miaka minne iliyopita kuhusu dawa hiyo.

Watafiti kutoka Taasisi ya Utafiti wa Dawa Kenya (Kemri), Marekani na Sweden wamesema wanawake wanaotumia dawa ya mpango wa uzazi ya Depo Provera wapo katika hatari kubwa ya kupata maambukizi ya Ukimwi.

Timu ya watafiti huo, imefanya uchunguzi kwa wanawake 228 Jijini Nairobi, baadhi yao wakitumia dawa ya Depo Provera pamoja na dawa zingine za mpango wa uzazi, ambapo wanawake waliotumia Depo Provera walikuwa na maambukizi zaidi ya Ukimwi ikilingani na waliotumia dawa nyingine.

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni