.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumatano, 25 Machi 2015

MAMA MMOJA ASHIKILIWA NA POLISI MAREKANI BAADA YA KUKUTWA NA MIILI YA WATOTO KWENYE JOKOFU

Mama mmoja huko Detroit nchini Marekani amekamatwa na polisi baada ya miili ya watoto wawili kukutwa ikiwa kwenye jokofu nyumbani kwake.

Maafisa wa Mahakama waliokuwa wakitekeleza amri ya kuhamishwa mama huyo hapo jana, walibaini miili hiyo ya mtoto wa kiume wa miaka 11 na mtoto wa kike wa miaka 14.

Polisi wa Detroit hawakutaja jina la mwanamke huyo lakini wamesema miili hiyo ilikuwa imevingirishwa kwenye mfuko mmoja wa plastiki.

Watoto wengine wawili wa mwanamke huyo wenye umri wa miaka 11 na 17, waliokutwa kwenye nyumba ya jirani, wamechukuliwa na kuhifadhiwa mahala salama na serikali.

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni