.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumanne, 24 Machi 2015

NDEGE YA SHIRIKA LA NDEGE LA UJERUMANI YAANGUKA NCHINI UFARANSA IKIWA NA ABIRIA 142

Ndege ya Shirika la Ndege la Ujerumani la German-wingsaina aina ya Airbus A320 ikiwa na abiria 142 na wahudumu wa ndege sita imeanguka nchini Ufaransa kati ya eneo la Barcelonnette na Digne.

Maafisa wa Mamlaka ya Usalama wa Ndege nchini Ufaransa kwa kushirikiana na polisi imesema ndege hiyo ilikuwa ikitokea Barcelona kwenda mji wa Dusseldorf nchini Ujerumani. Ndege hiyo inamilikiwa na shirika mama la Lufthansa.

Rais wa Ufaransa Francois Hollande amesema haijabainishwa jinsi ajali hiyo ilivyotokea lakini inapelekea kufikiria kuwa hakuna mtu aliyenusurika kwenye ajali hiyo. 
 

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni