.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Ijumaa, 13 Machi 2015

PICHA ADIMU ZA OSAMA BIN LADEN AKIWA ANAISHI MILIMA YA TORA BORA ZATOLEWE

Picha adimu za kiongozi wa Al Qaeda marehemu Osama Bin Laden zimetolewa akiwa anaishi katika maeneo ya milima ya Tora Bora kabla ya kutimuliwa kwa mashambulio ya anga yaliyomfanya akimbie makazi hayo kufuatia shambulio la Septemba 11.

Picha hizo zimetolewa wakati wa kesi ya kushirikiano na Al Qaeda inayosikilizwa Jijini New York Marekani, inayomkabili Luteni Khaled al-Fawwaz aliyetumika kama njia ya mawasiliano kwa taasisi ya kigaidi Jijini London katika miaka ya 1990.

Picha hizo zilipigwa na mwandishi wa Palestina Abdel Barri Atwan, ambaye alikaribishwa kwenye maficho hayo mwaka 1996 kama sehemu ya mpango wa Bin Laden kusambaza ujumbe wa chuki dhidi ya nchi za magharibi.
                                             Osama Bin Laden akiongea na mwandishi al-Suri
                                                               Osama Bin Laden akitabasamu
                Hapa Osama akiwa ndani ya pango akiongea na mwanshishi al-Suri

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni