.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Ijumaa, 13 Machi 2015

SERIKALI YA KENYA KUMLIPIA MATIBABU MUIGIZAJI MKONGWE MZEE OJWANG'

Naibu Rais wa Kenya William Ruto amesema serikali ya Kenya italipa gharama zote za matibabu ya muigizaji mkongwe wa vichekesho Mzee Ojwang'.

Muigizaji huyo ambaye jina lake halisi ni Benson Wanjau, amekuwa akisumbuliwa na tatizo la macho kutoona vizuri pamoja na kisukari na siku ya jumatano alilazwa kwenye Lions SightFirst Eye iliyopo Loresho.

Kwa mujibu wa madaktari wanaomtibu Mzee Ojwang' anatarajiwa kufanyiwa upasuaji wa macho hii leo.

Naibu Rais wa Kenya, kupitia akuanti yake ya twitta amesema serikali itamlipia matibabu Mzee Ojwang' na kumtakia apone haraka.

Taarifa za kuugua muigizaji huyo wa kundi la Vitimbi zilisambaa mitandaoni, huku mitandao ya jamii ikianzisha kampeni ya kumlipia gharama za matibabu kwa kutumia #OkoaMzeeOjwang.

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni