.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumanne, 24 Machi 2015

SHOW YA #MBAR2015 ELEGANZA YAFANA DAR ES SALAAM, SERENA HOTEL

‘Model’ wa kiume, kike watia fora na mavazi ya ubunifu ‘run way’ yabamba ndani ya dakika 20.  

Na Andrew Chale wa Modewji blog 

Ile shoo maalum ya mwaka iliyokuwa ikisubiriwa kwa hamu kubwa hatimaye usiku wa Machi 21 ndani ya Serena Hotel jijini Dar es Salaam, shoo hiyo ‘Mercedes Benz Ally Remtullah 2015 Eleganza’ imeweza kuwa ya aina yake na ya kipekee  kwa kuvutia kila mmoja aliyehudhuria shoo hiyo.

 Kama kawaida yake mbunifu wa mavazi, Ally Remtullah amekuwa akifanya vizuri kila mwaka kwenye shoo zake hizo anazoziandaa ambapo kwa shoo ya mwaka huu imezidi kuingia kwenye historia  kwa kuonyesha toleo jipya ‘New collection 2015’.

 Miongoni mwa mambo yaliyoweza kubamba katika shoo hiyo ni pamoja na  jukwaa ‘Run way’  kwa Models hao kulitendea haki na na kuonekana tukio la Kimataifa.

 Ni dhahiri shoo hiyo kwa kila aliyeshuhudia asilimia 100, ni ya Kimataifa. Ambapo ilichukua ndani ya dakika  20 huku kila Model  akipangilia vilivyo na mavazi maalum hali iliyopelekea kuliteka jukwaa.

 Aidha,  kwa upande wake Ally Remtullah alipongeza wadau wote kwa kuendelea kumuunga mkono ambapo aliiambia Modewji blog kuwa baada ya hapo anatarajia kuendelea kufanya maonyesho zaidi ikiwemo ndani na nje ya nchi.

 Pia aliwashukuru wadhamini akiwemo mdhamini Mkuu, Kampuni ya CFAO Motors LTD wauzaji wa magari kupitia brand yake ya Mercedes Benz.  Wengine ni  MeTL Group kupitia bidhaa za ki-elekroniki za LG  na wengine wengi.

 Fuatana na camera ya modewji blog kwa picha za 'Cat walk' ndani ya hoteli ya Serena jijini Dar es Salaam.






















Hakuna maoni :

Chapisha Maoni