.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumatano, 12 Agosti 2015

RAILA APONDA MAKUBALIANO YA KIBIASHARA BAINA YA UGANDA NA KENYA

Kiongozi wa chama cha upinzani cha CORD, Raila Odinga amemkosoa rais Uhuru Kenyatta kwa kutia saini makubaliano ya uagizaji sukari kutoka Uganda, na kutahadharisha kuwa yatauwa kabisa viwanda vya ndani vya sukari.

Raila pia amehoji makubaliano ya Kenya kusafirisha nyama pamoja na mazao ya maziwa nchini Uganda, kwa kusema kuwa mazao hayo mawili hayatoshelezi soko la ndani la Kenya kwa sasa iweje yasafirishwe nje ya nchi.

Katika kuonyesha upinzani kuponda makubaliano hayo ya kibiashara baina ya nchi za Kenya na Uganda, Odinga amesema kuwa masilahi binafsi ya biashara ndio yamewekwa mbele badala ya maslahi ya taifa.

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni