Watu 12 wameuwawa katika Jiji la
Cairo nchini Misri, baada ya bomu linalowaka moto kurushwa kwenye
hoteli.
Tukio hilo limetokea eneo la Agouza
katika jiji la hilo la Cairo kwa mujibu wa vyombo vya habari vya
Misri.
Gazeti la The Cairo Post limesema
watu waliofunika nyuso zao walirusha bomu hilo kwenye ukumbi ambao
pia una klabu ya usiku na kisha kukimbia.

Hakuna maoni :
Chapisha Maoni