Mchezaji wa Brazil Neymar
anatarajiwa kutoa ushahidi katika mahakama nchini Hispania kuhusina
na tuhuma za kujipatia fedha kwa njia za udanganyifu katika uhamisho
wa kujiunga na Barcelona.
Rais wa sasa na wa zamani wa klabu
hiyo ya Hispania wamekanusha kufanya kosa lolote Jijini Madrid hapo
jana.
Barcelona imesema ililipa euro 57m
(£43m) kwa Neymar mwaka 2013, wazazi wake wakipata euro 40m na klabu
ya Brazilian ya Santos euro 17m.
Hata hivyo wapelelezi wanasema ada
yake ilifikia karibu euro 83m na Barcelona walificha sehemu ya
makubaliano yao.
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni