.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumatatu, 23 Mei 2016

M/KITI SERIKALI YA MTAA MKOANI MWANZA AUAWA AKISULUHISHA WANANDOA

                                              Kamanda wa Mkoa wa Mwanza Ahmed Msangi

Baada ya siku sita tangu waumini wawili akiwamo Imamu wa msikiti wa Rahmani, Feruzi Eliasi, uliopo Ibanda Relini Kata ya Mkoloni jinamizi la mauaji hayo mkoani Mwanza limezidi kutisha baada ya jana usiku, Mwenyekiti wa mtaa wa Bulale kata ya Buhongwa, kuuawa kwa kupigwa risasi.

Tukio hilo lililotokea juzi saa 2 usiku, lilimkumba Mwenyekiti huyo, Alphonce Mussa (48), mkazi wa Bulale kata ya Buhongwa wilaya ya Nyamagana jijini Mwanza, aliyepigwa risasi mbili na watu wawili wasiojulikana wakati akijaribu kusuluhisha mgogoro wa ndoa kati ya Neema Marangula na mumewe.

Akisimulia tukio hilo kwa majonzi huku akiangua kilio, mke wa marehemu, Getrude Henrico, alisema wakati tukio hilo linatokea hakuwepo nyumbani kwani wakati huo alikuwa bustanini, alisimuliwa tukio hilo alipofika nyumbani.

Hata hivyo, mjane huyo alisema kabla ya tukio hilo, siku za karibuni waliuwa mbwa wao saba waliokuwa wanalinda mifugo, hivyo anahisi tukio hilo la mauaji ya mumewe yanaendana kabisa na kuuliwa kwa mbwa hao.

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni