.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumapili, 5 Juni 2016

WATU WENGI WAKARIBISHWA KUMZIKA MUHAMMED ALI SIKU YA IJUMAA

Maziko makubwa yatafanywa ya bondia mkongwe bora duniani Muhammed Ali siku ya Ijumaa ili kuruhusu kila mtu ambaye angependa kutoa heshima za mwisho kwa mwili wa Ali, familia yake imesema.

Maziko hayo ya Ali yatafanyika kwenye mji wa nyumbani kwao wa Louisville, Kentucky, ambapo kwa mujibu wa ratiba rais wa zamani wa Marekani Bill Clinton amepangwa kusoma wasifu wa Muhammed Ali.

Katika orodha ya wazungumzaji wakati wa maziko ya Muhammed Ali, pia yupo Mchekeshaji Billy Crystal, mwandishi wa habari za michezo Bryant Gumbel.

Bondia huyo mkongwe bingwa wa uzito wa juu mara tatu alifariki dunia Ijumaa akiwa na umri wa miaka 74, kwa kifo cha kawaida kilichosababishwa na ugonjwa ambao bado haujabainishwa.
                    Rais wa zamani wa Marekani Bill Clinton akiwa na Muhammed Ali
                                            Rais Barack Obama akisalimiana na Muhammed Ali
               Mtoto aliyefika kuomboleza kifo cha Muhammed Ali akiweka shada la maua
Muombolezaji akiwa amepiga goti kwa hisia kali katika eneo la kuweka mashada ya maua huko Louisville, Kentucky.

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni