.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumapili, 5 Juni 2016

MANCHESTER UNITED YATOA OFA YA PAUNDI MILIONI 30 KWA BEKI ERIC BAILLY

Klabu ya Manchester United ya Uingereza imetenga dau la paundi milioni 30 ili kumnasa beki wa kati wa timu ya Villarreal raia wa Ivory Coast, Eric Bailly, ambaye anaaminika kuwa anakiwango cha juu.

Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 22, alikuwa anafuatiliwa kwa karibu na timu za Manchester City, Bayern Munich na Arsenal katika siku za hivi karibuni lakini Manchester United ndio wamekuwa wa kwanza kutoa dau.

Bailly aliyeachwa katika kikosi cha Ivory Coast kilichoivaa Gabon hapo jana, pia timu za Barcelona na Leicester zilikuwa zikimfuatilia tangu Januari lakini Villarreal wanaimani kuwa anaweza akaenda Manchester United. 
                                                             Beki Eric Bailly akiwa kibaruani dimbani

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni