.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumamosi, 28 Januari 2017

SERENA WILLIAMS AMFUNGA DADA YAKE VENUS NA KUWA NAMBA MOJA DUNIANI

Serena Williams amemfunga dada yake Venus kwa seti mbili mfululizo na kushinda taji lake la saba la Mashindano ya Tenesi ya Wazi ya Australia, na kuweka rekodi ya Grand Slam ya 23.

Serena, 35, amemshinda Venus, 36, kwa seti 6-4 6-4 na kumshinda Steffi Graf aliyekuwa akiongoza kwa kushinda mara nyingi mashindano makubwa ya wachezaji wa kulipwa mwaka 1968.

Kwa ushindi huo Mmarekani huyo aliyekuwa anashikilia namba mbili kwa ubora duniani katika uchezaji tenesi, sasa amekuwa namba moja dunia akimpiku Mjerumani Angelique Kerber.
Serena Williams akinyanyua kombe alilochukuwa huku dada yake Venus akiangalia
Wanadada ndugu Serena na Venus Williams wakikumbatiana baada ya kumalizika kwa mchezo wao wa fainali
                Serena Williams akiwa amekaa chini akishangilia kwa furaha baada ya kushinda 

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni