.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumamosi, 28 Januari 2017

KAMPUNI YA GOOGLE YAITA WAFANYAKAZI WAKE WAREJEE MAREKANI

Kampuni ya Google imewaita wafanyakazi wake waliosafarini kurejea Marekani, badaa rais Donald Trump kutoa amri ya kuzuia raia wa mataifa saba ya Kiislam kuingia Marekani.

Katika agizo hilo wakimbizi kutoka Syria wamezuiwa kuingia Marekani hadi hapo itakapotolewa agizo jingine.

Raia wa mataifa sita ya kigeni yakiwemo ya Iran na Irak watazuiliwa kuingia Marekani kwa muda wa siku 90.

Pia programu yote ya kuandikisha wakimbizi imesitishwa kwa siku 120 na kiwango cha chini cha kuchukua wakimbizi kimeshushwa.

Jumamosi abiria kadhaa wa Irak na Yemeni walizuiliwa kuingia kwenye ndege katika uwanja wa ndege wa Cairo kuelekea Jijini New York, licha ya kuwa na visa za Marekani.
               Waandamanaji wakipinga sera za kuwabagua wahamiaji za rais Donald Trump

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni