.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumamosi, 28 Januari 2017

TIMU YA LIVERPOOL YATOLEWA NJE KOMBE LA FA NA TIMU YA WOLVES

Timu ya Wolves imepambana kiume na kuiduwaza Liverpool kwa kuitundika magoli 2-1 na kutinga raundi ya tano ya kombe la FA katika mchezo uliochezwa kwenye dimba la Anfield.

Richard Stearman aliwafanya wageni Wolves waongoze ndani ya sekunde 53, baada ya kuachwa bila ya ulinzi na kuunasa mpira wa adhabu wa Helder Costa.

Costa alimtengenezea nafasi Andreas Weimann aliyemzunguka kipa wa Liverpool, Loris Karius na kuifanya Wolves kuongoza kwa magoli mawili kabla ya mapumziko.

Mchezaji mwenye asili ya Kenya Divock Origi aliifungia Liverpool goli pekee la dakika za mwisho.
                                             Richard Stearman akifunga goli kwa mpira wa kichwa 
                                Andreas Weimann akimzunguka kipa wa Liverpool na kufunga goli 
                                       Mshambuliaji Divock Origi akifunga goli pekee la Liverpool 

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni