.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Alhamisi, 16 Februari 2017

BAYERN MUNICH SI YA MCHEZO MCHEZO YAIPA ARSENAL 'MKONO'


Matumaini ya Arsenal katika Ligi ya Mabingwa Ulaya yanaelekea kuparanganyika baada ya kukubali kupata kipigo ukome kunijua cha magoli 5-1 kutoka kwa Bayern Munich, katika mchezo wa kwanza wa hatua ya 16.

Arsenal ambayo imekuwa ikitolewa katika michuano hiyo katika hatua ya mtoano mara sita katika misimu ya nyuma si tu ilikubali kipigo cha mkono, pali pia ilishuhudia ikizidiwa na Bayern Munich ambayo ilimiliki mpira kwa asilimia 75.

Katika mchezo huo Alexis Sanchez alirekebisha makosa yake ya kukosa kufunga kwa mkwaju wa penati, na kufunga goli lililosawazisha goli lililofungwa na Arjen Robben kwa shuti bora la umbali wa yadi 25.

Arsenal ilimkosa Laurent Koscielny aliyeumia katika kipindi cha pili, huku Bayern ilicharuka ndani ya dakika 10 ambapo Robert Lewandowski alifunga kwa kichwa huku Thiago Alcantara akifunga mara mbili na kisha Thomas Muller kukamilisha karamu ya magoli.
                                            Arjen Robben akifunga goli la kwanza katika mchezo huo 
                             Alexis Sanchez akifunga goli pekee la Arsenal katika mchezo huo

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni