.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumatano, 15 Februari 2017

PARIS ST-GERMAIN YAFANYA MAAJABU YA MWAKA YAICHAKAZA BARCELONA

Angel di Maria amefunga mara mbili wakati Paris St-Germain ikiipa kipigo cha paka mwizi timu ya Barcelona na kuifanya kuwa katika hatari kutotinga hatua ya robo fainali ya Ligi ya Mabingwa Ulaya kwa mara ya kwanza katika muongo mmoja.

Katika mchezo huo ambao PSG iliutawala mno, ilipata goli lake la kwanza kwa mkwaju wa kuzungusha wa adhabu uliopigwa kiufundi na Di Maria, na kisha Julian Draxler aliongeza goli la pili.

Wakati Barcelona ikijiuliza Di Maria tena akafunga goli la tatu kwa shuti la kuzungusha na mpira ukajaa kwenye kona ya juu ya goli, kabla ya Edinson Cavani kukamilisha ushindi huo kwa kufunga goli la nne na kufanya matokeo kuwa 4-0.
                              Angel di Maria akipiga kiufundi mpira wa adhabu uliozaa goli la kwanza
                                  Julian Draxler akijipinda na kufunga goli la pili katika mchezo huo

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni