.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Alhamisi, 23 Machi 2017

UJERUMANI YATIBUA REKODI YA KOCHA WA UINGEREZA SOUTHGATE

Kocha Gareth Southgate amepata kipigo cha kwanza wakati Uingereza ikizamishwa kwa goli 1-0 dhidi ya Ujerumani kwa goli lililofungwa kiufundi na Lukas Podolski katika kipindi cha pili.

Southgate alikuwa hajafungwa katika michezo minne tangu aitwae Uingereza kutoka kwa kocha Sam Allardyce, na kushuhudia machungu hayo kutoka kwa mabingwa wa kombe la dunia.

Katika mchezo huo Adam Lallana alipiga mpira uliogonga mwamba wa goli na shuti la Dele Alli lilizuiwa na kipa Marc-Andre ter Stegen, katika kipindi cha kwanza.
     Lukas Podolski akiwa haamini goli alilofunga kwa kufunika kwa mikono uso wake
                                 Jamie Vardy akiwa amevaana na kipa Marc-Andre ter Stegen

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni