.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumapili, 2 Aprili 2017

CRYSTAL PALACE YAIFANYA MAAJABU YA KUIFUNGA CHELSEA NYUMBANI

Uongozi wa Chelsea katika Ligi Kuu ya Uingereza umepungua na kuwa tofauti ya pointi saba, baada ya kupata kipigo cha kushtusha nyumbani cha magoli 2-1 kutoka kwa Crystal Palace huku Tottenham ikiifunga Burnley.

Kikosi cha Antonio Conte kilikuwa kimeshinda michezo yao 10 iliyopita katika dimba la Stamford Bridge na kilikuwa hakijapoteza nyumbani katika michuano yoyote ile tangu Septemba 16, kabla ya kipigo hicho.

Katika mchezo huo Chelsea ilikuwa ya kwanza kuona nyavu baada ya Cesc Fabregas kutumbukiza kimiani mpira wa krosi ya Eden Hazard baada ya dakika tano tu ya mchezo lakini wakajikuta wanapoteza mapema.

Wilfried Zaha aliyekuwa katika kiwango chake alifanya jitihada binafsi na kusawazisha goli kwa shuti la sekonde 91 na baadaye akamtengenezea nafasi ya kufunga Christian Benteke na kuifanya Crystal Palace kupata goli la pili.
                         Eden Hazrad akifunga goli pekee la Chelsea katika mchezo wa jana
            Wilfred Zaha akijipinda na kuachia shuti lililojaa wavuni na kusawazisha goli
                 Christian Benteke akifunga goli la pili na la ushindi kwa Crystal Palace 

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni