.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumapili, 2 Aprili 2017

TOTTENHAM YAIFUNGA BURNLEY NA KUISOGELEA CHELSEA

Tottenham imepunguza pengo na vinara wa Ligi Kuu ya Uingereza Chelsea na kuwa pointi saba baada ya baada ya kuifunga timu ngumu ya Burnley kwa magoli 2-0 katika dimba la Turf Moor.

Wageni Tottenham walihaha kusaka goli na hatimaye jitihada zao zilizaa matunda baada ya kupata goli kupitia kwa Eric Dier baada ya wenyeji kushindwa kuizuia krosi ya Christian Eriksen.

Vincent Janssen, alijikuta akiingia katika orodha ya majeruhi watatu wa Tottenham baada ya kuumia akicheza mchezo wake wa kwanza wa Ligi Kuu msimu huu na nafasi yake kuchukuliwa na Son Heung-min ambaye alifunga goli la pili.
                                                             Eric Dier akifunga goli la kwanza la Tottenham
                                                       Son Heung-min akifunga goli la pili la Tottenham 

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni