.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumapili, 2 Aprili 2017

LIVERPOOL YAZIDI KUPAMBANA KUBAKIA NAFASI NNE ZA JUU

Liverpool imeongeza nafasi ya kujihakikisha kumaliza katika nafasi za juu nne za msimamo wa Ligi Kuu ya Uingereza baada ya kuifunga Everton kwa magoli 3-1.

Sadio Mane aliipatia Liverpool goli la kuongoza baada ya kugongeana vyema na Roberto Firmino na kuachia shuti lililokwenda kujaa kwenye kona ya goli.

Matthew Pennington aliifungia Everton goli la kusawazisha likiwa ni goli lake la kwanza akiwa na Everton akicheza kwa mara ya kwanza katika msimu huu.

Coutinho aliwatoka wachezaji wa Everton na kufunga kwa shuti la kuzungusha na kisha baadaye akamtengenezea Divock Origi aliyetokea benchi na kufunga goli la tatu.
                           Sadio Mane akiachia shuti na kufunga goli la kwanza la Liverpool 
               Countinho akipiga shuti la mpira wa kuzungusha na kufunga goli la pili 
                            Sadio Mane akichezewa rafu na Tom Davies ambaye alipewa kadi 

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni