Dar Es Salaam, April 2017:
DMG Tanzania, kampuni tanzu ya chakula na vinywaji nchini, imezindua
bidhaa yenye mchanganyiko wa kahawa, maziwa na sukari ya “Nuru coffee
Chapchap” yenye hadhi ya kimataifa na ladha thabiti.
Uzinduzi
huu umekuja wakati muafaka kufuatia changamoto mbalimbali za kiuchumi
zinazoendelea nchini ikiwa na dhumuni la kulenga kila Mtanzania kuonja
ladha mpya ya Nuru coffee Chap chap ikipatikana nchini kote nchini na
katika masoko yote.
Kutokana
na ubunifu wa DMG Tanzania unaowatofautisha na wapinzani wake katika
soko, kampuni hii imewawezesha Watanzania hata ya hali ya chini, kuwa
na uwezo wa kuonja ladha murua yenye mchanganyiko wa maziwa, sukari na
kahawa kwa gharama nafuu kabisa ya Tsh 500=/
Akizungumzia bidhaa hiyo mpya ,Bw. Rayton Kwembe Mkurugenzi wa Nuru Coffee Chapchap anasema “ Nuru
coffee Chapchap ni bidhaa ya kipekee na ni moja kati ya bidhaa
madhubuti katika kampuni yetu. Nuru ni neno la Kiswahili linamaanisha
“mwangaza” ikiwa na maana ya asili, Nishati, na matumaini . Nuru huondoa
giza na kuweka dhahiri vitu vilivyofichika. Nuru hung’aa popote na
kurudisha tumaini kwa watu waliokata tamaa.”
Hivyo
uzinduzi wa kahawa ya Nuru coffee Chapchap imekuja kwa wakati muafaka
na kutoa fursa za kujikwamua kiuchumi kutokana na fursa za ajira
zinazotolewa nchini na kampuni hii na
pia bidhaa ya nuru coffe imekuwa nuru kwa watanzania kwani
imewawezesha kujipatia chai yenye mchanganyiko wa sukari maziwa na
kahawa kwa gharama nafuu kabisa kwa kuzingatia hali yetu uchumi.
“Tunayofuraha
kubwa kuzindua bidhaa hii ya kiwango cha juu itakayokidhi maisha ya
mtumiaji, kwa kumpatia ladha nzuri ya kahawa bora kabisa na chapchap.
Nuru coffee Chapchap inatokana na aina mbili kuu za kahawa nchini,
Robusta na Arabika kwa asilimia 100 na kutengenezwa kwa mchanganyiko
madhubuti wa maziwa na sukari, ili kuleta ladha nzuri ya kuvutia.
Tumejipanga na tuna ujasiri mkubwa juu ya bidhaa yetu mpya na hivyo
hatutatetereka.” Alisema ,Bw. Rayton Kwembe Mkurugenzi wa kampuni hiyo.
Hivi
sasa Nuru coffee Chapchap inapatikana katika mikoa ya Dar es Salaam,
Mwanza, Shinyanga, Mbeya, Dodoma na Arusha, na pia bidhaa hii
inatarajiwa kupatikana mikoa mingine nchini miezi michache baadae.
Katika
kusherekea uzinduzi wa Nuru Coffee Chapchap katika soko la nchini
Tanzania kampuni ya DMG Tanzania imeandaa kampeni itakayohusisha
supamaketi kubwa mbalimbali kama TSN Supermarkert iliyopo kibo complex,
American Super Markert pugu road na Nakumatt Mlimani City. Kampeni hiyo
pia itahusisha upatikanaji wa nuru Coffee katika mitaa mbalimbali
katika jiji la Dar es Salaam kuanzia tarehe 16 – 25 Aprili mwaka huu.
Kitu
kikubwa Zaidi katika bidhaa ya Nuru coffe ni utaalamu wa usindikaji wa
bidhaaa hiyo na ufungaji wa paketi zake zinazolenga kuibua hisia ya
mtumiaji kabla hata hajainunua.
Nuru
coffee Chapchap wafurahia kumtaja na kumtambulisha George Sixtus Mdemu,
(G Nako) ambaye ni mwanamuziki wa kizazi kipya “maarufu kama Bongo
Fleva” kuwa balozi wa bidhaa ya Nuru Coffee Chapchap nchini Tanzania. G
Nako atakuwa akiitangaza bidhaa ya Nuru coffee Chapchap katika soko la
Tanzania pamoja na vyombo vya habari kama radio, TV, magazeti na
mitandao ya kijamii.
Pamoja
na mambo mengine G Nako kama balozi wa Nuru coffee Chapchap atakuwa
akishirikiana pamoja na wateja wetu kueneza bidhaa yetu yenye ubora wa
hali ya juu.
“Tunayo
furaha kubwa na tunategemea G Nako ataeneza uwezo wa bidhaa yetu na
kuwa balozi madhubuti. Tunajivunia kazi tunayoendelea kufanya pamoja
naye na tunategemea kuimarisha uhusiano wetu kwa kuikuza lebo yetu na
kuieneza kote nchini” Alisema Bw. Rayton Kwembe Mkurugenzi wa kampuni hiyo.
“Mimi
pamoja na Nuru coffee Chapchap tumekuwa na uhusiano thabiti, DMG
Tanzania ni kampuni nzuri na ninajivunia kufanya kazi pamoja nayo, “ G Nako.
DMG
Tanzania haitabaki nyuma katika kuhakikisha inaongeza ubora katika
bidhaa yake ya Nuru coffee Chapchap na pia inampango wa kuzindua bidhaa
nyingine nyingi chini ya mwamvuli wa lebo ya Nuru. Ikiwa na lengo la
kukuza usambazaji wa bidhaa yake DMG Tanzania inalenga kuifikia Tanzania
yote pamoja na Africa Mashariki.
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni