.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Ijumaa, 21 Aprili 2017

KOCHA WA TIMU YA TOTTENHAM U23 UGO EHIOGU AFARIKI DUNIA

Nyota wa zamani wa Uingereza na Aston Villa, Ugo Ehiogu, amefariki dunia leo baada ya jana kupatwa na shambulizi la moyo katika viwanja vya mazoezi vya Tottenham.

Kocha huyo wa Tottenham kwa wachezaji chini ya miaka 23, alianguka jana asubuhi katika uwanja wa maozoezi wa timu hiyo na kupatiwa huduma ya haraka na madaktari wa Tottenham.

Madaktari wahuduma ya kwanza waliitwa na alikimbizwa hospitali kwa gari la wagonjwa, lakini alifariki dunia mapema leo akiwa na umri wa miaka 44.
Kocha Ugo Ehiogu akiwa na mkewe Gemma pamoja na mtoto wao wa kiume wakati wa uhai wake

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni