.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumapili, 2 Aprili 2017

RAIS MALINZI AZIPONGEZA TIMU ZA JKT OLJORO, MAWENZI NA TRANSIT CAMP

Rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), Jamal Emil Malinzi amezipa kongore timu za JKT Oljoro ya Arusha, Mawenzi ya Morogoro na Transit Camp ya Shinyanga kwa kufanikiwa kupanda daraja baada ya kufanya vema kwenye hatua ya Nne Bora (Play off) iliyofikia kikomo jana Aprili mosi, mwaka huu.

Katika salamu zake za pongezi, Rais Malinzi amezitaka timu hizo sasa kujiimarisha katika nyanja za usajili na maandalizi mengine ili kuwa timu za ushindani katika Ligi Daraja la Kwanza (FDL) ambako watashiriki kuanzia msimu mpya utakaoanza Julai, mwaa huu.

“Nichukue nafasi hii kuzipongeza timu zote ambazo zimepanda daraja kutoka Ligi Daraja la Pili na kwenda Ligi Daraja la Kwanza. Pongezi nyingi ziwaendee wanafamilia wote kuanzia viongozi, wachezaji, waamuzi walioamua mechi zao, mashabiki nakadhalika,” amesema Malinzi na kuongeza:

“Huu ni uthibitisho kuwa timu zote ziliajianda vya kutosha na kupata matokeo,naamini hata Cosmopolitan nayo ilijiandaa lakini kwa bahati mbaya pointi hazijatosha kwa msimu huu. Ni imani yangu kuwa itapambana msimu ujao na kufanikiwa.”

Kadhalika Rais Malinzi alizitakia kila la kheri timu zote katika kumaliza msimu na kuanza msimu ujao.

NI SERENGETI BOYS NA BLACK STARLETS KESHO UWANJA WA TAIFA

Timu ya Taifa ya Tanzania ya vijana wenye umri wa chini ya miaka 17 maarufu kama Serengeti Boys, kesho Jumatatu itapambana na Black Starlets ya Ghana kwenye mchezo wa kirafiki wa kimataifa utakaofanyika Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.

Katika mchezo huo utakaoanza saa 10.00 jioni, Serengeti Boys itautumia kama ni ishara ya kuwaaga mamilioni ya Watanzania kabla ya kusafiri kwenda kwenye fainali za Kombe la Mataifa ya Afrika kwa vijana zitakazofanyika Gabon kuanzia Mei 14, mwaka huu.

Lakini kabla ya kutua Gabon, Serengeti Boys itakwenda Rabat, Morocco kufanya kambi ya takribani mwezi mmoja kuanzia Aprili 5, mwaka huu. Ikiwa huko angalau itacheza mechi za kirafiki zisizopungua mbili dhidi ya wenyeji morocco na timu nyingine ya jirani ama Tunisia au Misri. Kambi hiyo ya Morocco itamalizika Mei mosi, mwaka hu ambako timu itasafiri hadi Cameroon.

Ikiwa Cameroon, timu itacheza mechi mbili za kirafiki za kimataifa dhidi ya wenyeji yaani Mei 3 na 6, mwaka huu kabla ya kusafiri Mei 7, mwaka huu kwenda Gabon ambako Serengeti Boys imepangwa kundi B pamoja na timu za Mali, Niger na Angola.
Vipimo vya mechi dhidi ya Ghana kadhalika hapo baadaye Cameroon, vitakuwa mwafaka kwenye kufanya tathmini ya uwezo wa Serengeti Boys kwani wapinzani hao wamekuwa na rekodi nzuri kwenye soka la vijana na kwa kipindi hiki zimepangwa kundi A pamoja na wenyeweji Gabon na Guinea.

Kila la kheri Serengeti Boys katika mapambano ya kuwania ubingwa wa Afrika kadhalika kucheza fainali za Kombe la Dunia hapo Novemba, mwaka huu zitakazofanyika India. Serengeti Boys inaweza na Mtanzania tunakuomba kuichangia timu hii kwa namna ya 223344 kupitia mitandao yote ya simu.

IMETOLEWA NA SHIRIKISHO LA MPIRA WA MIGUU TANZANIA

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni